Historia ya Hospitali ya Mt. Francisco, hospitali teule ya wilaya
- 1921 Kuwasili kwa masista wa kwanza wa “Baldegg” kutoka Uswiss
- 1927 Kufunguliwa kwa zahanati

Dispensari ya zamani inatumika kama maktaba
- 1931 Kufunguliwa kwa hospitali ikiwa na vitanda 30
- 1937 Kujengwa kwa wodi ya wazazi
- 1951 Daktari mmisionari anaanza rasmi kazi yake huko Ifakara
- 1953 Daktari wa upasuaji kutoka Austria Zams, Dr. Karl Schöpf anakuja Tanganyika na familia yake na anakuwa daktari mpya mmisionari
- 1955 Ujenzi wa hospitali mpya ya Mt. Fansisco ulianza
- 1957 Kufunguliwa kwa kituo cha utafiti kutoka Uswiss chenye taasisi ya magonjwa ya ukanda wa kitropiki
- 1960 Kufunguliwa kwa hospitali mpya ya Mt. Fransisco
- 1961 Tanganyika inakuwa huru chini ya Julius Nyerere kama rais wa kwanza. Kwa kuungana na Zanzibar nchi inaitwa TANZANIA

Hospitali ya wakoma "Nazareti" imekuwa makao ya walemavu wengi na waliokuwa zamani wagonjwa wa ukoma.
- 1967 Kufunguliwa kwa hospitali ya wakoma “Nazareti” iliyobuniwa na Mhandisi Norbert Heltschl kutoka Tyroler. Ilifadhiliwa na jimbo la Innsbruck chini ya Askofu Dr. Paulus Rusch. Katika mwaka huo huo Rais Nyerere alitangaza “Azimio la Arusha”
- 1969 Dr. Schöpf anahitimisha kazi yake Tanzania na kurejea Zams. Katika miaka iliyofuata wataalam mbalimbali wa tiba kutoka Uswiss na Ujerumani walichukua nafasi ya ukurugenzi wa hospitali
- 1976 Hospitali inakuwa chini ya serikali na hivyo kuwa hospitali ya wilaya za Kilombero na Ulanga,mmiliki akibakia kuwa jimbo katholiki la Mahenge
- 1993 Dr. Patience L. Kibatala anachukua nafasi zote mbili ya ukurugenzi wa hospitali na ukuu wa idara ya upasuaji akiwa Mtanzania wa kwanza.
- 1995 Mwaka 1995 - Mwanzo wa ushirikiano kati ya hospitali ya Zams na hospitali ya Mt. Fransis
- 2004 Mwaka 2004 - Kuanzishwa kwa "Ushirika wa marafiki wa Ifakara"


